Bwana Anakuja

Bwana Anakuja
Performed by-
CategoryMajilio (Advent)
ComposerF. A. Nyundo
Views14,941

Bwana Anakuja Lyrics

  1. Bwana anakuja, twendeni kumlaki,
    Bwana Mungu wa Majeshi
    Ziwasheni nyoyo, tumkampokee,
    huyu mwenye utukufu

    Karibu Bwana njoo, Karibu Bwana njoo
    Shinda pamoja nasi

  2. Wewe ndiwe mkate, mkate wa mbinguni,
    utulishe wenye njaa
    Wewe ndiwe mwanga, sisi tu vipofu,
    tufanye tuone tena
  3. Wewe ndiwe njia, tutakufuata,
    turudi kwa Baba yetu,
    Wewe ni ukweli, utuangazie,
    tusije tukapotoka
  4. Wewe ni uzima, sisi tu wagonjwa,
    twakujia utuponye
    Tumwendee nani, tukielemewa,
    kitulizo chetu wewe
  5. Wewe ni mzabibu, sisi tu matawi,
    tuungane siku zote
    We mchungaji mwema, tunakutambua,
    tuongoze malishoni
  6. Bado tu njiani, yadumu imani,
    tumaini na upendo
    Saa ya kufa kwetu, tupate kuona,
    uso wako wa rehema