Harusi Kidededede

Harusi Kidededede
Performed bySt. Anthoney Malindi
AlbumMalindi Kuna Nini
CategoryHarusi
ComposerAlfred Ossonga
Views28,997

Harusi Kidededede Lyrics

  1. { Bwana harusi na bibi harusi, leo mmefunga ndoa ya maisha,
    Kaeni kwa amani kidededede } * 2

    Upendo wenu umedhihirika
    Uyani kwenu bamba ishini tototo
    Uzuri wenu hauna kifani
    Uyani kwenu bamba ishini tototo
    Na nyumba yenu imebarikiwa
    Uyani kwenu bamba ishini tototo ooo

  2. Jitulize mjisikie sukari, siku ya leo ni yenu,
    Furahini, mmepambwa maua mnapendeza
  3. Bwana arusi kwanza wachangamka, bibi arusi chachawa,
    Chezacheza, penzi lenu leo limekamilika
  4. Mapenzi yenu yote yatasitawi, hakika yatasitawi,
    Yatamea, kama ule mwerezi wa Lebanoni
  5. Baraka zake Mungu ziwashukie, kaeni pasipo shida,
    Siku zote nyumba yenu iwe hekalu la Mungu.