Hebu Jiulize

Hebu Jiulize
Performed bySt. Cecilia Mirerani
AlbumMchanganyo
CategoryTafakari
ComposerE. A. Minja
Views5,981

Hebu Jiulize Lyrics

  1. {Hebu jiulize lingetolewa tangazo leo
    Ya kwamba kila apumuaye
    na ailipie pumzi avutayo } *2
    Ni nani angejificha asilipe kodi,
    Ni nani angesema yeye ni masikini,
    Ni nani angekwepa kwani yeye ni tajiri
    Ni nani angekuwa kweli mtu wa kiburi
    Ni nani angekwepa kweli kulipia kodi (nasema)
    Ni nani angependa kunyang'anywa uhai wake * 2

  2. Tazama sasa majirani zako wote,
    Hakuna unayeongea naye
    Kwani unawadharau
    kwa kuwa wao hawana fedha kama zako
    Hebu tazama baadhi ya ndugu zako,
    Hupendi hata kuwaona kwako
    Unawakana kwa kuwa, wao ni maskini,
    tena unawaona ni wachafu.
  3. Kwa nini hivyo, biashara zako,
    wewe unawaajiri wafanya kazi
    Tena ni wachapa kazi na mwisho wa mwezi,
    huwafichia eti wameiba
    Hebu tazama wapoteza fedha nyingi,
    unapokuwa baa na marafiki
    Kwa ajili tu ya anasa, na kuwasaidia,
    maskini kwako ni hasara
  4. Jitafakari, fungua na legeza moyo wako
    kwa kuwajali wasiojiweza
    Na wenye shida mbalimbali, na sio kuegeza
    Hazina ya moyowe kwa shetani.