Hii Ndiyo Siku

Hii Ndiyo Siku
Performed byOur Lady of Fatima Kongowea
AlbumKila Mwenye Pumzi (vol 4)
CategoryEntrance / Mwanzo
Views8,730

Hii Ndiyo Siku Lyrics

  1. Hii ndiyo siku, aloifanya Bwana *2
    Tuishangilie, na kuifurahiya *2
    {Tupige makofi na vigelegele
    Sote turuke juu tumshukuru Mungu } *2

  2. Ndiwe Mungu wangu nami nitakushukuru
    Ndiwe Mungu wangu nami nitakutukuza
    Nitakushukuru kwa moyo wangu wote
    Kwa mema yote Bwana uliyonijalia
  3. Nifungulieni malango ya haki,
    Nitaingia mimi na kumshukuru Mungu
    Nitakushukuru kwa moyo wangu wote
    Kwa mema yote Bwana uliyonijalia
  4. Mkono wa kuume wa Bwana umetukuzwa
    Mkono wa Bwana hutenda makuu
    Nitakushukuru kwa moyo wangu wote
    Kwa mema yote Bwana uliyonijalia
  5. Mshukuruni Bwana kwa kuwa yeye ni mwema
    Kwa maana fadhili zake ni za milele
    Nitakushukuru kwa moyo wangu wote
    Kwa mema yote Bwana uliyonijalia