Hii ni Ekaristi

Hii ni Ekaristi
Performed bySauti Tamu Melodies
AlbumZilipendwa
CategoryEkaristia (Eucharist)
Composer(traditional)
VideoWatch on YouTube
Views31,432

Hii ni Ekaristi Lyrics

  1. Hii ni ekaristi, aliyotuachia
    Bwana Yesu Kristu (Kristu)
    Mkombozi wa dunia

    { (imbeni) Imbeni kwa furaha
    (sifuni) Sifuni ekaristi
    (alimo) Alimo Yesu Kristu (Kristu)
    Alimo ni mzima } *2

  2. Yesu katuonea, wema pia huruma
    Alitupenda sana (sana)
    Akatupa uzima
  3. Jioni Alhamisi, alichukua mkate
    Kaugeza mwili (mwili)
    Kuleni mkaokoke
  4. Pia alichukua, kikombe cha divai
    Kaigeuza damu (damu)
    Kunyweni mkaokoke
  5. Walipokwisha kula, kawaosha miguu
    Nimewapa mfano (mfano)
    Fanyeni nanyi vile
  6. Yesu mwili na damu, chakula cha uzima
    Tujaliwe kupata (pata)
    Uzima wa milele.