Kama Kunguru

Kama Kunguru
Performed bySt. Paul Students' Choir (University of Nairobi)
AlbumHabari Tuliyoleta (Vol 6)
CategoryTafakari
ComposerJ. C. Shomaly
Views4,351

Kama Kunguru Lyrics

  1. { Kama kunguru arukapo juu ya jalala kubwa
    Akitafuta mizoga na wadudu
    Alishibishe tumbo lake } *2

    { Ndivyo moyo wake mtu asiyempenda Mungu
    Utakuwa wa kubabaika na kuhangaika
    Hatakuwa na amani,
    Atakuwa kama kunguru tu, kama kunguru tu,
    Awindaye toka macheo ya jua hata yapata mawio
    Na tumbo lake bado ni tupu } *2

  2. Moyo wako ndugu mbona waubabaisha,
    Kutwa kucha wewe umemsahau Mungu
    Dunia ina mambo yake - tena yanapita
  3. Kama una kiu na tamaa za dunia
    Zina mwisho wake kwanza mtafute Mungu
    Mungu alishapanga yako - hivyo umuombe