Kila Kunapokucha

Kila Kunapokucha
Performed by-
CategoryTafakari
Views3,728

Kila Kunapokucha Lyrics

  1. { Kila kunapokucha, ndugu zangu mimi
    Wananikwepa na kunikimbia
    Majirani zangu wanatazamana bila kunitamkia neno
    Ewe Muumba wangu najiuliza na kujitafakari mimi
    Au nimekuwa na sura ya simba,
    Au nimekuwa na sura ya chui, hata ninatisha } *2

  2. Ninapokaa chini na kutafakari mwenendo wangu
    Kwani uko vipi mimi niliupenda,
    Japo magumu mimi niliyapata,
    Nilivaa sura ya kifalme pasipo kuwa na utu
  3. Nikiupekua pekua moyo wangu unanitisha
    Ni huo tena kwa kudhamiria
    Kwa kauli toka kwa ulimi wangu
    Nilifanana na jitu baya tena limezalo watu
  4. Hakuna adui hakuna rafiki kwangu wote sawa
    Hakuna mwema katika moyo wangu
    Wala rafiki katika roho yangu
    Nilijifananisha na chui tena chui mwenye njaa