Lo Kaburi Wazi

Lo Kaburi Wazi
Performed byOur Lady(Star of the Sea) Kenya Navy
AlbumTumeandamana
CategoryPasaka (Easter)
ComposerAlfred Ossonga
Views8,977

Lo Kaburi Wazi Lyrics

  1. Mama Maria tuambie, uliona nini njiani
    Nanyi mitume tueleze mliyemkuta pangoni
    { (kweli) Ni malaika, toka mbinguni
    Tulimwona pale kaburini } *2

    Lo! Kaburi wazi!
    Hayumo, ni mzima, hayumo, amefufuka *2
    Lo! Kashinda kifo!
    Mauti, yameshindwa, tuimbe, tushangilie *2

  2. Amefufuka ni hakika, amefufuka kweli kweli
    Dunia nzima ifurahi, hata mbinguni wanaimba
    { (kweli) Twimbe tucheze, twimbe turuke,
    Twimbe sana , twimbe aleluya } *2
  3. Nguvu za shetani kashinda, kamba za mauti amekata
    Ngome ya kuzimu kavunja, kaburi za wafu zafunguka
    { (kweli) Simba wa Yuda, amenguruma,
    Walinzi nao mbio watimua } *2
  4. Ameondoka kaburini, aelekea Galilaya
    Nasi twendeni hima hima, twendeni kule Galilaya
    { (kweli) Twendeni leo, twendeni sote,
    Tumwimbie nyimbo za ushindi } *2
  5. Tumekombolewa kwa damu, damu yake Mwanakondoo
    Lango la mbingu liko wazi, kwao waliokombolewa
    { (kweli) Tukimwamini, tutaingia,
    Tutaishi na Mungu milele } *2