Mfalme wa Amani

Mfalme wa Amani
Performed bySt. Joseph Cathedral Dar-es-Salaam
CategoryJumapili ya Matawi (Palm Sunday)
Composer(traditional)
Views14,972

Mfalme wa Amani Lyrics

  1. Mfalme wa amani mpeni heshima,
    Yerusalem mjini anaingia
    Na unyenyekeo na upole mkuu
    Anapanda punda Mwana wa Mungu.

    Hosana juu, hosana Juu, hosana juu.

  2. Njooni Mahebruni, njooni watoto,
    Leteni matawi ya kumsalimu.
    Mwana wa Daudi kweli Masiya
    Anakuja kwenu mwenye huruma.
  3. Tandikeni nguo miguuni pake,
    Imbeni zaburi, shangilieni.
    Mbarikiwa huyu ajaye kwetu
    Kwa Jina la Bwana Mkombozi mkuu.
  4. Ufurahi sana, we` Yerusalem
    Yule wamwabudu roho za mbingu.
    Na huruma pale anakujia,
    Haki na amani akuletea.
  5. Ndimi za wachanga zafumbulia,
    Kwa mwujiza sifa yake Masiya
    Na makundi yote ya malaika
    Sifa na heshima wanamtolea.