Moyo Wangu Wamtukuza

Moyo Wangu Wamtukuza
Performed by-
CategoryBikira Maria
Views39,289

Moyo Wangu Wamtukuza Lyrics

  1. {(Moyo) Moyo wangu wamtukuza Bwana
    (Roho) Roho yangu inafurahi }*2

  2. Kwa kuwa amemwangalia, kwa huruma mtumishi wake
    Hivyo tangu sasa watu wote, wataniita mwenye heri
  3. Kwa sababu Mwenyezi Mungu, amenifanyia makuu
    Jina lake ni takatifu,
  4. Huruma yake ni kwa wote, wote wale wanaomcha
    Kizazi hata na kizazi,
  5. Huyatenda mambo makuu, kwa nguvu za mkono wake
    Wenye kiburi hutawanywa,
  6. Hushusha wote wenye vyeo, kutoka vitini vya enzi
    Nao wale wanyenyekevu, wote hao huwainua
  7. Huwashibisha wenye njaa, na matajiri huwaacha
    Waende mikono mitupu,
  8. Hulilinda taifa lake, teule la mtumishi wake
    Akikumbuka huruma yake,
  9. Kama alivyowaahidia, babu zetu kuwaahidia
    Ibrahimu na mzao wake,
  10. Atukuzwe Baba na Mwana, naye Roho Mtakatifu
    Leo kesho hata milele, kwa shangwe milele amina

    ~Lk. 1:39-55
Also recorded by Thika Catholic