Mpende Adui

Mpende Adui
Alt TitleAmri ya Mapendo
Performed bySt. Cecilia Kajiado
AlbumImani Kipimo
CategoryLove
ComposerM. Z. Yohana
Views6,949

Mpende Adui Lyrics

  1. Bwana Yesu alituachia amri ya mapendo
    Ili tupendane kama yeye alivyotupenda
    Tena akasema, akasisitiza,
    Mpende jirani, kama nafsi yako

    { Mpende - adui yako
    Mpende - muombee neema
    Mpende - adui yako
    Mpende - muombee Baraka } *2

  2. Sisi tulivyoumbwa wanadamu hatulingani
    Kwa tabia kwa maisha hata kwa matendo yetu
    Wapo wa hekima, wasemao ukweli,
    Na wenye kiburi, wasio na busara
  3. Hata ukinyanyaswa jitahidi kuvumilia
    Usiwe mwenye ghadhabu ukalipiza kisasi
    Ukihuzunishwa, mkimbilie Yesu,
    Atakupa faraja, heri na fanaka
  4. Usikumbuke ubaya uliokwisha tendewa,
    Hiyo itakuwa njia ya kukaribisha chuki
    Ukisha samehe, usahau yote,
    Ukatae yote, yasiyo ya hekima