Nakuja na Zawadi

Nakuja na Zawadi
Alt TitleNaondoka Mimi
Performed bySt. Anthoney Malindi
AlbumMalindi Kuna Nini
CategoryOffertory/Sadaka
ComposerAlfred Ossonga
Views29,453

Nakuja na Zawadi Lyrics

  1. Naondoka mimi naenda kwa Baba,
    Nipeleke hiki nilichokipata,
    Japo kidogo, sitaona haya,
    Nimeamua, sitarudi nyuma

    { Nakuja polepole Baba,
    Nakuja na zawadi yangu
    Naleta mbele zako ili nitoe shukurani } *2

  2. Natembea mimi mwendo wa madaha,
    Nakanyaga chini kwa maringo tele,
    Naelekea, altare ya Bwana,
    Nimkabidhi, nilichojaliwa.
  3. Nimechangamka ninashangilia,
    Napiga kelele kelele za shangwe
    Nachezacheza, najongea kwako,
    Ee Mungu Baba Nipokee mimi.
  4. Nafsi yangu mimi naileta kwako,
    Mkate divai pia ninaleta
    Uigeuze, mwili na damuyo,
    Chakula chetu, tunaosafiri
  5. Mavuno shambani mimi nimevuna,
    Mifukoni fedha nimekabidhiwa,
    Mimi ni nani, nisikushukuru,
    Baba nasema asante kwa yote.