Ngoja Nicheze

Ngoja Nicheze
Performed bySt. Kizito Makuburi
AlbumMungu Yule
CategoryEntrance / Mwanzo
ComposerBernard Mukasa
Views8,906

Ngoja Nicheze Lyrics

  1. Tazama mimi ninavyopumua,
    Tazama mimi nilivyo na nguvu
    Tazama mimi ninavyopumua,
    Tazama mimi nilivyo na nguvu
    Hizo zote - ni neema bure toka kwa Mungu
    Na mimi leo - ngoja nicheze muone,
    Nitamsifu ngoja nicheze muone,
    Bila kuchoka - ngoja nicheze muone aee

  2. Tazama mimi nakula na kushiba,
    Tazama mimi nalala nasinzia
    Tazama naamka mimi mwenyewe e,
    Tazama tazama ah tazama aa aha
  3. Tazama mimi naweza kuongea,
    Tazama mimi naimba bila shida
    Tazama naweza kucheza mwenyewe e
    Tazama tazama ah tazama aa aha
  4. Nikiugua ona napewa pole,
    ninapofiwa ndugu mwanifariji
    Tazama niwapo na shida wanajaa a
    Tazama tazama ah tazama aa aha
  5. Nikikosea huwa nasamehewa,
    Nikiudhiwa ndugu mwanitetea
    Tazama dhuluma haitaniua a
    Tazama tazama ah tazama aa aha
  6. Nikifurahi ndugu washerehekea,
    Nikiudhiwa ndugu wasononeka
    Tazama ninaishi kati ya watu u
    Tazama tazama ah tazama aa aha
  7. Na yote haya najaliwa na Mungu,
    Amenipenda upeo wa upendo
    Tazama na mimi nitamtukuza a
    Tazama tazama ah tazama aa aha