Nikulipe Nini

Nikulipe Nini
Performed bySt. Anthoney Malindi
AlbumMalindi Kuna Nini
CategoryOffertory/Sadaka
ComposerAlfred Ossonga
Views14,547

Nikulipe Nini Lyrics

  1. Nikulipe nini ewe Mungu Baba wa Mbinguni
    Kwani mtu mimi sina kitu cha kujivunia

    Uhai na nguvu ni zawadi nzuri umenipa wewe Baba.
    Maisha mazuri ni talanta safi nimepata kwako wewe
    Sasa nakuomba baba nigeuze chombo chako
    Nimejitolea kwenda kutangaza neno lako *2

  2. Nikufananishe na nini humu ulimwenguni
    Uliumba vyote bahari mito hata milima
  3. Ningekuwa ndege hakika ningeruka angani
    Ningekuwa nyota ningemulika dunia yote
  4. Nitakutendea nini ili nikufurahishe,
    Nitakuimbia wimbo gani Baba nikusifu
  5. Unitume Baba popote nipeleke ujumbe
    Nitalihubiri Jina lako daima milele