Nikupe Nini Mungu Wangu

Nikupe Nini Mungu Wangu
Performed bySauti Tamu Melodies
AlbumZilipendwa
CategoryOffertory/Sadaka
ComposerBasil Lukando
VideoWatch on YouTube
Views48,899

Nikupe Nini Mungu Wangu Lyrics

  1. { Nikupe nini Mungu wangu, nikupe nini we Mwokozi
    Nikupe nini Bwana wangu cha kukupendeza } *2

  2. Kila nitakachoshika mbona bado ni kidogo
    Fadhili unazotenda kwangu mimi naogopa
    Ninakuomba Mwokozi, nifanyie msamaha na unipokee
    Mema unayoyatenda, nitafanya nini mimi nikurudishie
  3. Nakutolea mkate toka mmea wa ngano
    Nakutolea divai ni tunda la mzabibu
    Ninakuomba Mwokozi . . .
  4. Mchana hata siku wewe wanisimamia
    Na nikiwa safarini waniepusha ajali
    Ninakuomba Mwokozi . . .
  5. Nikiwa na matatizo Bwana wanisaidia
    Nikiwa kwenye majonzi Bwana unanifariji
    Ninakuomba Mwokozi . . .
  6. Kama njia siioni Bwana unaniongoza
    Na hata nikipotea kwako unanirudisha
    Nitatoa nini mimi, kitakachokuwa sawa, na fadhili zako
    Nitaimba vipi mimi, niyataje mema yote, utendayo kwangu