Ninaikumbuka Siku

Ninaikumbuka Siku
Performed bySt. Cecilia Mirerani
AlbumMchanganyo
CategoryTafakari
ComposerE. A. Minja
Views9,785

Ninaikumbuka Siku Lyrics

  1. Ninaikumbuka siku ile niliyokuita Bwana wangu
    Ukaniponya na kuniepusha na hatari mbaya ya kifo
    Mwili wangu uliopatwa na majeraha makubwa
    Yenye maumivu makali na ya kutisha
    Na ya kukatisha tamaa

    {
    /b/
    Nitamke maneno gani, niimbe wimbo gani mimi
    Nicheze ala gani au niipige ngoma gani
    Kama asante na shukrani yangu Bwana
    Na nitoe sadaka gani, iwe kama shukrani yangu
    Nikikumbuka wema wako, nisifuje Bwana wangu
    Wewe ni mwenye huruma na upendo

    /w/
    Maneno gani mimi nitamke, na wimbo gani niimbe
    Mimi nipige ngoma gani
    kama asante na shukrani yangu Bwana
    Sadaka nikutolee ee Bwana,
    ni kama shukrani yangu, nikusifuje Bwana wangu,
    Wewe ni mwenye huruma na upendo } * 2

  2. Ninakumbuka siku ile mimi niliposhindwa
    Na maumivu ya majeraha ya kichwa niliyoyapata
    Maumivu makali mimi yalinibana sana
    Hata mwili ulikosa nguvu na fahamu kunipotea
    (Mimi ) mimi Bwana (niseme) niseme asante
    Kukushukuru ee Mungu wangu
    (Mimi) mimi Bwana (nisipo) nisipotamka nitakuwa sina fadhila
  3. Ninakumbuka siku ile mikono yangu mimi
    Ilipopatwa na maumivu yaliyotokana na ajali
    Mikono yangu mimi ilitokwa na damu nyingi
    Hata na mifupa yangu iliyovunjika na kutokeza
    (Mimi ) mimi Bwana (niseme) niseme asante
    Kukushukuru ee Mungu wangu
    (Mimi) mimi Bwana (nisipo) nisipotamka nitakuwa sina fadhila
  4. Nilipopata fahamu nikajaribu kusimama
    Mwili ulikosa nguvu kwa maumivu tena makali
    Miguu yangu inatokwa damu nyingi na kunitisha
    Hata na mifupa yangu iliyovunjika na kutokeza. . .
    (Mimi ) mimi Bwana (niseme) niseme asante
    Kukushukuru ee Mungu wangu
    (Mimi) mimi Bwana (nisipo) nisipotamka nitakuwa sina fadhila
  5. Usingizi mzito ulinibeba na kunifanya
    Niyasahau maumivu yangu yote niliyo nayo
    Maumivu makali tena ya ndani yalinibana
    Hata kuhema siwezi kugeuka hadi nisaidiwe . . .
    (Mimi ) mimi Bwana (niseme) niseme asante
    Kukushukuru ee Mungu wangu
    (Mimi) mimi Bwana (nisipo) nisipotamka nitakuwa sina fadhila
  6. Hebu jiulize ndugu ni wangapi wanaopata haya
    Hata uhai wao hutoweka na usirudi
    Jitafakari ndugu wewe uzima uliojaliwa
    Hata asante kwake Muumba tazama umemsahau, .
    (Mimi ) mimi Bwana (niseme) niseme asante
    Kukushukuru ee Mungu wangu
    (Mimi) mimi Bwana (nisipo) nisipotamka nitakuwa sina fadhila