Niseme Nini Basi

Niseme Nini Basi
Performed bySt. Joseph Migori
AlbumNitachezacheza
CategoryBikira Maria
ComposerAlfred Ossonga
Views30,931

Niseme Nini Basi Lyrics

  1. { Niseme nini basi juu ya mama Yetu Maria
    (Mama Bikira Maria)
    Mama mpendelevu mama mwenye neema } *2

  2. Wakati wa majaribu, mwombezi wetu ni Maria (Mama yetu)
    Wakati wa mashaka kimbilio letu ni Mama (Maria)
  3. Mama uliyeumbwa, pasipo dhambi ya asili
    Ukamzaa mwanao mkombozi wa walimwengu
  4. Moyo wako wa heri moyo safi moyo mweupe
    Nijalie neema nishinde majaribu yote
  5. Mama wa Mkombozi mnara wetu wa Mbinguni
    Mwangaza wetu sisi tunaosafiri gizani
  6. Shika mkono wangu unionyeshe njia ya kweli
    Nifike kwa Mwanao anakoketi uwinguni