Njooni tumwimbie Bwana wetu - kwa shangwe
Njooni kwa masifu kwa nderemo - tucheze
{Njooni tuabudu, njooni tusujudu
Tupige makofi,
Mbele zake Bwana, Mungu wa ulimwengu } *2
- Hekalu lake Bwana Mungu linapendeza,
Nyumbani mwake Bwana mna mengi mazuri
Ninatamani kuingia nyumbani mwake
Nikae naye siku zote nyuani mwake
Nipate heri, mbele za Bwana
- Mapema leo ninabisha lango ee Bwana
Nifungulie nipokee nipe faraja
Nimelemewa na mizigo mingi ya dhambi
Nyumbani mwake Bwana ndiko kuna uzima
Uzima tele, na usalama
- Twendeni sote kwake Bwana Mungu Mwenyezi
Twendeni kwake tupeleke maombi yetu
Tutoe shukrani zetu kwa Mungu Baba
Tutoe na dhabihu zetu kwake Muumba
Sadaka zetu, azipokee
- Uhai wetu unatoka kwake Muumba
Tuimbe sifa zake Mungu siku kwa siku
Tuyatangaze maajabu yake popote
Tuseme Bwana ametenda mambo makuu
Kwa watu wote, milele yote.
|
|
|