Safari ya Mafanikio

Safari ya Mafanikio
Performed bySt. Cecilia Mirerani
AlbumMchanganyo
CategoryTafakari
ComposerVictor Aloyce Murishiwa
Views8,089

Safari ya Mafanikio Lyrics

  1. Safari ya mafanikio ni ngumu sana
    Ukiwa na imani haba itakushinda
    Unapoianza safari bahari imetulia
    Unapata matumaini ya kumaliza salama
    Ukifika katikati mambo hubadilika
    Ni mawimbi na vikwazo misukosuko mingi
    Usikate tamaa, jipe moyo utashinda * 2

  2. Utapata machukizo na matatizo mengi
    Ndiyo hali ya dunia, yote uvumilie
    Utapata mitihani, migumu ya maisha
    Ndiyo hali ya dunia, yote uvumilie
  3. Utapata vishawishi vingi vya ulimwengu
    Ndiyo hali ya dunia vyote uvumilie
    Utapata marafiki wema nao wabaya
    Ndiyo hali ya dunia wote wavumilie
  4. Utapata masumbuko na maradhi ya ajabu
    Ndiyo hali ya dunia yote uvumilie
    Kaza mwendo ndugu yangu
    kaza mwendo kwenye nuru
    Songa mbele e Mkristu yote uvumilie