Sasa ni Wakati Mzuri

Sasa ni Wakati Mzuri
Performed bySt. Paul Students' Choir (University of Nairobi)
AlbumIkatetemeka Nchi (Vol 3)
CategoryOffertory/Sadaka
ComposerF. Mtegeta
Views7,406

Sasa ni Wakati Mzuri Lyrics

  1. Sasa ni wakati mzuri twendeni madhabahuni,
    Tukatoe sadaka zetu, tulijenge kanisa la Mungu
    { Ewe ndugu yangu mkristu,
    Changamka, changamka, peleka sadaka kwa Bwana.
    Nenda katoe kwa moyo mweupe
    Uzipate baraka za Mungu } *2

  2. Mkristu kutoa sadaka,
    Ndio wajibu wa kila mmoja,
    Hivyo mkristu kumbuka wajibu,
    Nenda katoe sadaka kwa Bwana.
  3. Mwambie Bwana Mungu wako,
    Baba pokea nilichokileta,
    Hiki ndicho ulichonijalia,
    Nakutolea kama shukrani.
  4. Zamani za mababu zetu,
    Walipeleka sadaka za nyama,
    Nasi wakristu wa leo twendeni,
    Tupeleke fedha za mifukoni.