Tazama Tazama

Tazama Tazama
Performed by-
CategoryTafakari
Views16,338

Tazama Tazama Lyrics

  1. { Tazama tazama ni vyema na vizuri
    Ndugu kuishi pamoja kwa umoja } *2

  2. Mapendo ya Kristu yametuunganisha
    Ndugu tuishi pamoja kwa mapendo
  3. Tumshangilie na tufurahie kwake
    Tumche tumpende Mungu mzima Bwana
  4. Kristu Bwana Mungu tunakuomba leo
    Tupe neema tukupende wewe
  5. Tunapokusanyika kwa pamoja daima
    Tuangalie tusitengane tena

    * * *
  6. Mapendo ya Kristu yametuunganisha,
    Ndugu kuishi pamoja kwa umoja
  7. Tuwe na furaha tunapokusanyika,
    Kwa moyo mnyofu tusameheane kweli,
  8. Na tuangalie tusitengane kamwe,
    Tuache ugomvi tujenge mapatano
  9. Kati yetu sisi akae Yesu Kristu,
    Yeye ni kiungo cha wanadamu wote,
  10. Awaunganishe waliotengana nasi,
    Tuwe kundi moja mchungaji ndiye mmoja.
  11. Tunapokusanyika kwa pamoja
    Tuangalie tusitengane tena
  12. Kristu Bwana Mungu tunakuomba leo
    Tumiminie neema ya kupendana
  13. Kanisa letu na yale ya wenzetu
    Tuungane pamoja tunakuomba