Wosia

Wosia
Alt TitleMkimtumainia Mungu
Performed byKwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha
AlbumMSHIPI (VOL. 22)
CategoryTafakari
ComposerG. C. Mkude
Views11,239

Wosia Lyrics

  1. Tulieni ndugu zangu niwaambie siri moja
    Mkimtumainia Mungu mtayashinda yote
    Japo magumu ni mengi mtakayokutana nayo
    Mkimtumainia Mungu mtayashinda yote

    { Mtavuka vikwazo vya shetani na magumu yote (nasema)
    Mbinu zake shetani na hila hazitawaangusha (nasema)
    Mkimtumainia Mungu mtayashinda yote } *2

  2. Kwa nguvu za Mwenyezi nasema hamtaaibika-
    Mtautimiza huu wito wenu kikamilifu -
  3. Mungu Baba yuko nyuma yenu anawapigania-
    Atawafukuza na maadui wenye hila mbaya .
  4. Wosia ninawapa ndugu muwe na uvumilivu-
    Kwani haya ya dunia si kitu wala si lolote .