Yesu Mwema Najitolea Kwako

Yesu Mwema Najitolea Kwako
Performed bySt. Augustine Bugando Mwanza
CategoryEkaristia (Eucharist)
Composer(traditional)
Views20,502

Yesu Mwema Najitolea Kwako Lyrics

  1. Yesu mwema najitolea kwako,
    Kwa leo hii na siku zote
    Nafsi yangu na moyo wangu wote
    Heri kweli, heri kweli, heri kweli raha ya uwingu *2
  2. Ndani mwangu umekuja daima,
    Kuwa nami ni pendo lako
    Ewe mpenzi mwenye utamu mwingi
    Ni mapendo, ni mapendo, ni mapendo ya moyo wako *2
  3. Nitaweza kukurudishia nini,
    Kwa wema huu na pendo lako
    Roho yangu umeifadhilia
    Nikupende, nikupende, nikupende ni tamaa yangu*2
  4. Weka Rabi katika roho yangu,
    Wema wako na unyenyekevu,
    Na pendo kuu fadhila ya imani
    Niongoze, niongoze, niongoze katika imani *2
Harmonized by Fr. Malema