Zungukazunguka

Zungukazunguka
Alt TitleMbinguni Kwa Baba
Performed bySt. Anthoney Malindi
AlbumMalindi Kuna Nini
CategoryTafakari
ComposerAlfred Ossonga
Views7,600

Zungukazunguka Lyrics

  1. Mbinguni kwa Baba, kweli kuna raha,
    Makerubi wote hata maserafi
    Malaika wote na watakatifu,
    Wako mbele za Mungu kila mtu na kazi yake

    Waimbaji tutaimbaimba, tutaimba nyimbo za shangwe
    Malaika watarukaruka, wataruka mbele za Mungu
    Watu wote (kweli) watafurahi nyumbani mwa Bwana
    Watacheza (wote) pamoja wakizungukazunguka

  2. Tuimbe nyimbo nzuri kama makerubi,
    Tuimbe kwa furaha kama maserafi
    Na tuchezecheze kama watakatifu,
    Tukirukaruka kama malaika wa Mungu
  3. Wenye moyo safi na matendo mema,
    Twendeni kwa Baba tupate dhawabu
    Tumekaribishwa Mbinguni kwa Baba
    Twendeni tuone, jinsi tulivyoandaliwa.
  4. Sisi tunaimba nyimbo za Mbinguni,
    Tena twatabiri yale ya Mbinguni
    Yote yalopita kwa wenye hekima,
    Tumefunuliwa, tutangaze kwa nyimbo hizi
  5. Fanya utafiti na upeleleze,
    Utafunuliwa siri za Mbinguni
    Waloshinda vita, wateule wa Mungu
    Wanatungojea kwenye raha ya siku zote