Nakushukuru Baba
Nakushukuru Baba Lyrics
- Nakushukuru Baba (shukuru), Baba Mwenyezi Mungu
Mwenyezi kwa kuwa umeniumba
Nakushukuru Baba (shukuru), Baba Mwenyezi Mungu
Mwenyezi kwa kuwa umeniumba
Nitakulipa nini ee Mungu, wangu cha kukupendeza wewe
Baba mimi sina kitu chochote
Cha kulinganisha na ukarimu wako
Maombi yangu uyapokee, na dua zangu zikufikie
Kwa huruma yako Baba nisamehe
Mimi kwa makosa niliyoyatenda
Tafadhali Baba uniongezee siku nyingi ili nikutumikie
- Nakutukuza Baba (tukuza), wewe ni ngome yangu
Ngome yangu ndiwe unayenilinda
Pokea sifa Baba (pokea) sifa ni zako wewe,
zako wewe Baba Mwenyezi Mungu
- Nakuabudu Baba (abudu), Baba Mlinzi wangu -
Mlinzi kwa kuwa wewe ni mwema
Uniongoze Baba (ongoze), katika kweli yako,
Kweli yako nifanye mapenzi yako
- Bwana nifanye mimi (nifanye), chombo cha kazi yako
kazi yako nikutumikie wewe
Pasipo na amani (pasipo), pasipo na upendo,
upendo nitangaze Jina lako
- Usiniache Baba (ee Baba), uwe nami daima
Daima katika maisha yangu,
Nikufuate wewe (fuate), daima siku zote,
siku zote milele hata milele