Utukufu (Misa Amecea)

Utukufu (Misa Amecea)
Performed by-
AlbumMisa Amecea
CategoryTBA
Views19,881

Utukufu (Misa Amecea) Lyrics

MISA AMECEA - UTUKUFU

  1. Utukufu kwa Mungu juu mbinguni
    Na amani kote duniani
    (Kwa watu) wenye mapenzi mema

    |s/a| Tunakusifu Baba, tunakuheshimu,
    Twakuabudu sisi tunakutukuza
    |t/b| Kusifu tunakusifu, heshimu,
    Twakuabudu abudu tunakutukuza
  2. Twakushukuru Mungu kwa ‘tukufu
    Wako mkuu ewe Mungu mfalme
    (Ee Baba) wa Mbingu Baba yetu
  3. Bwana wetu mwokozi Yesu Kristu
    Mwana wa pekee wake Mungu
    (Uliye) Mwanakondoo wa Mungu
  4. Unayeziondoa dhambi zote
    Za dunia utuhurumie
    (Pokea) pokea ombi letu
  5. Wewe unayeketi kuume
    Kwake Baba utuhurumie
    (Sikia) sikia ombi letu
  6. Kwani pekee yako ndiwe Bwana
    Pekee yako mkuu na mkombozi
    (Pekee) pekee Yesu Kristu
  7. Kwa umoja wa Roho mtakatifu
    Ndani yake Baba watukuzwa
    (Ee Yesu) milele na milele