Imeandikwa Wapi

Imeandikwa Wapi
Alt TitleNimefungua Vitabu Vyote
Performed bySt. Cecilia Mavurunza
AlbumNimefungua Vitabu Vyote
CategoryTafakari
ComposerVictor Aloyce Murishiwa
Views5,060

Imeandikwa Wapi Lyrics

  1. Nimefungua vitabu vyote nikapekua kurasa zote
    Kulitafuta andiko hili sikuliona
    Ni wapi palipohalalishwa matendo haya
    machafu sana yachafuayo jamii yetu sikupaona
    Fungua macho mkristu, fungua macho
    Giza nene limetanda, fungua macho
    Ni wakati wa kukesha, fungua macho
    Shetani katuzunguka, fungua macho
    Imeandikwa wapi kwamba ushoga ni halali?
    Wapi palipoandikwa rushwa ni funguo ya haki?
    (tena) Imeandikwa wapi kwamba hirizi ni halali?
    Wapi imehalalishwa wanaume kufunga ndoa?
    (hiyo) Imeandikwa wapi, imeandikwa wapi?
    Kurasa zote hakuna!
    Imeandikwa wapi imeandikwa wapi?
    Sheria zake Mungu!

  2. Kemea Mkristu matendo hayo
    Kwa sakramenti zote uyasafishe
    Epukana nayo matendo hayo
    Kwa sakramenti zake uyasafishe
  3. Ingia katika shamba la Bwana
    Mambo ya ulimwengu ni machafuko
    Tembea katika shamba la Bwana
    Zitende kazi zake kwa moyo safi
  4. Njia zake Bwana usiziache
    Ni barabara safi zenye amani.
    Sheria za Bwana usiziache
    Na maagizo yake ni ya Adili