Ni Wewe Tu

Ni Wewe Tu
Alt TitleKanuni Moja na Lugha Moja
Performed bySt. Veronicah Kariakoo
AlbumWalinizunguka Kama Nyuki
CategoryHarusi
ComposerBernard Mukasa
Views8,122

Ni Wewe Tu Lyrics

  1. Kanuni moja na lugha moja kwako we
    Siku zote nitakupenda kweli ee
    Ya ulimwengu hayanibadilishi we
    Siku zote nitakupenda kweli ee (haya)

    Katika raha, (ni wewe) katika shida, tena ni wewe tu * 2
    Ni wewe tu, ni wewe tu (tena ) ni wewe tena ni wewe tu * 2

  2. Tumefinyangwa kwa tope moja sisi ee
    Ni pumzi moja imetutengeneza ee
  3. Ingawa ulimwengu mtamu sana ee
    Sitaujali kwani wewe ni zaidi
  4. Mapungufu yako nitayachukulia
    Na msamaha sitakawia kukupa
  5. Nitakupenda kama nilivyoagizwa
    Kama Kristu alivyolipenda kanisa
  6. Maisha yetu yakamtukuze Baba
    Yamuinue Mwana yampambe Roho
Recorded by * St. Veronicah Kariakoo * Mt. Yuda Thadei Mbeya * Kapotive Singers Bukoba