Mwana wa Mungu

Mwana wa Mungu
Performed by-
CategoryKwaresma na Toba (Lent & Repentance)
Views6,904

Mwana wa Mungu Lyrics

  1. Mwana wa Mungu, Yesu Kristu,
    Bwana ninakuomba unisikie.
    Mimi mdhambi ninatubu.
    Bwana unisafishe na damu yako. *2

    { Bwana unisafishe, hakika sina wema
    (sina wema) bila neema yako,
    Mimi mwenyewe sina uwezo } *2

  2. Nina imani kwako Bwana,
    vile ulinifia msalabani.
    Ulichukua dhambi zangu,
    Ukanifungulia kwako mbinguni *2
  3. Mungu wa amani na mapendo,
    Mimi nitatukuza jina lako kuu
    Unishike mkononi,
    kazi yake shetani kutupoteza *2
  4. Na kazi yangu ikiisha, Bwana,
    Ninatamani kuja kwako juu,
    Niwe pamoja na wateule,
    Tukitumikia mpaka milele. *2