Asante Mungu Wangu

Asante Mungu Wangu
Performed by-
CategoryThanksgiving / Shukrani
Views9,500

Asante Mungu Wangu Lyrics

  1. Asante Mungu wangu asante,
    moyo wangu wakusifu Aleluya.

  2. Natamani rukaruka kama ndege,
    kwa furaha nifike huko mbinguni
    Natamani kuwika kama jogoo,
    Kuonyesha furaha niliyonayo
  3. Mungu wangu ni mkuu namtukuza,
    hansinzii na halali sikieni
    Ukilala yeye halali ni mlinzi wangu,
    Na mchana sambasamba twatembea
  4. Hunilisha huninywesha siku zote,
    Mungu wangu wa ajabu asifiwe
    Posho langu sitaona njaa kamwe,
    Maji yangu sitaona kiu kamwe
  5. Malaika juu mbinguni wanaimba,
    wakisema hosanna atukuzwe
    Wateule juu mbinguni wanaruka,
    Wateule duniani tufanyeje