Ni Siku Kubwa

Ni Siku Kubwa
Performed by-
CategoryHarusi
Views4,251

Ni Siku Kubwa Lyrics

  1. Ni siku kubwa njooni nyote tushangilieni
    Kweli kwa shangwe na tupigeni vigelegele
    Twaomba Mungu Baba Awabariki awajalie na watoto
  2. Ni siku kuu ya harusi siku ya furaha
    Kwani wawili wamepatana kufunga ndoa
    Lindeni ndoa yenu Ili kwa dhiki wala faraja msitengane
  3. Mungu alipomuumba mwanamume Adamu
    Akamuumbia mwanamke waishi pamoja
    Agano lake Mungu Msilivumje, msilitupe, mhifadhi.
  4. Basi wewe mwanamume umpende mke wako
    Umlinde na kumtunza asiwe na upweke
    Umlinde siku zote Hadi mwenyezi Mungu atakapoamua
  5. Na wewe mwanamke umpende mume wako tu
    Na watoto mtakaojaliwa naye Mungu
    Uwatunze kwa wema, na kanisani uwapeleke kwake Mungu