Uniokoe Uniokoe

Uniokoe Uniokoe
Performed by-
CategoryTafakari
Views3,115

Uniokoe Uniokoe Lyrics

  1. Unioke uniokoe na watu hao wabaya
    Na unikinge unikinge na wakatili
    Wenye mawazo mabaya *2

  2. Daima hao huzusha ugomvi
    Na ndimi zao hatari kama nyoka
    Midomo yao maneno hatari
    Ni kama sumu hatari ya joka
    Mwenyezi Mungu naomba unilinde
    Kwa kucha zao wabaya na katili
  3. Wenye kiburi hutega
    Mipango yao waone uanguke
    Wametandaza kamba kama wavu
    Njiani wamezificha mitego
    Mipango yao yote wanikamate
    Sauti ya ombi langu sikiliza
  4. Mkombozi mkuu wangu umenikinga
    Salama hata wakati wa vita
    Waovu usiwape wanayotataka
    Mipango yao mibaya huivunje
    Wameinua kucha wamenizingira
    Uovu wao wenyewe uwapate