Nilikuomba Unipe
Nilikuomba Unipe |
---|
Performed by | - |
Category | Tafakari |
Views | 2,244 |
Nilikuomba Unipe Lyrics
- Nilikuomba unipe (nipe) nguvu nipate kufanikiwa
Nawe ukanipa udhaifu nipate kumnyenyekea Mungu
Nilikuomba unipe (nipe) afya nitende mambo makubwa
Nawe ukanipa maradhi nitende mambo mema zaidi
Asante Mungu (twakushukuru) kwa wema wako wote
Maana wewe u mwema, umenihurumia umenijalia mema yote
Umeninyima yote (mabaya) ukanijalia yote (haya)
Maana nayahitaji, umenihurumia umenijalia mema yote
{Nasema ee Mungu - Na sasa ee Mungu wangu mpenzi
Na sasa ee Mungu - Napenda kukiri neno hili moja
Kati ya watu - Kati ya watu wa ulimwengu
Nimebarikiwa - nimebarikiwa mno ee Mungu asante} *2
- Nilikuomba nipe utajiri nipate kujaa furaha
Nawe ukanipa ufukara nipate kuishi kwa busara
Nilikuomba nipe mamlaka wapate kunisifia
Nawe ukanipa udhaifu nipate kumhitaji Mungu
- Nilikuomba nipe kila kitu nifurahie maisha
Nawe ukanipa uhai nivifaidi vitu vyote
Nilikuomba unipe na ujanja nionekane hodari
Nawe ukanifanya mjinga nijifunze kumtii Mungu
- Nilikuomba nipe maarifa nipate kujulikana
Nawe ukanifanya mnyonge nipate kumtumaini Mungu
Nilikuomba unipe enzi nipate kumiliki nchi
Nawe ukanitia majonzi nipate kumkimbilia Mungu