Nyumbani Mwake Bwana
Nyumbani Mwake Bwana Lyrics
Nyumbani mwake Bwana tuingie kwa furaha.
Twendeni tumwabudu tunjongee mbele zake. *2
- Njoni tumsujudu yeye aliyetuumba
Yeye anatawala kwa haki na uamini.
- Yeye ni Mungu mwenye utukufu wa ajabu
Yeye ni Mungu mwenye radhi nyingi na rehema.
- Bwana ni mtawala amejaa utukufu na mashuhuda
Yake yastahili imani.
- Yeye ni Mungu wetu wa amani na mapendo
Yeye ni Mungu mwenye utukufu wa ajabu.
- Tumpigie shangwe mwamba wa wokovu wetu
Ni Mungu wa ujuzi na ni Mungu wa fahamu.
- Na kwa nyimbo za sifa tujongee uso wake
Vifijo na nderemo tumsifu Mungu wetu
- Na enyi waadili tukuzeni jina lake
Mfanyieni shangwe yeye aliyetuumba.