Ahadi

Ahadi
Performed byBMT Ledochowska K/Ndege Dodoma
AlbumSinodi Afrika
CategoryTafakari
ComposerChristian Charles
Views4,657

Ahadi Lyrics

  1. Niliyafumbua macho yangu nikatazama,
    Ili nimuone ashukapo toka winguni
    Maana aliniahidi kuwa atarudi
    Kunichukua tukafurahi pamoja naye Mbinguni

    Ilikuwa hamu ya moyo wangu tazama
    Na bado ninatamani kipi kitanizuia
    Niuone uso wa Bwana na Mungu wangu
    Nimuone akiitimiza ahadi yake

  2. Kaniahidi nikivumilia mpaka mwisho
    Nitamuona katika kiti chake cha enzi
    Akanionya nijitenge mbali na wazushi
    Wasije wakaipotosha imani yangu, hakika
  3. Nijapoanguka katika dhambi ya mauti
    Ataiosha ikawa nyeupe kama suti
    Na tena nikimlilia katika ukunga
    Atanipa uzao kama nyota za mbinguni, ajabu
  4. Kwa hiyo moyo wangu umetulia kabisa
    Kwa kuwa nimejua kwamba ipo tumaini
    Atukuzwe Baba Mwana na Roho Mtakatifu
    Kama ilivyo mwanzo, sasa na milele yote amina