Wewe ni Mungu

Wewe ni Mungu
Alt TitleSikia Sauti Yangu
Performed bySt. Kizito Makuburi
AlbumMimina Neema
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerBernard Mukasa
Views61,213

Wewe ni Mungu Lyrics

  1. // u t a n g u l i z i //

    Sikia aa sikia Bwana,
    Sikia aa sikia Bwana sauti yangu
    Sikia aa sikia leo
    Sikia aa sikia Bwana sauti yangu.

    Hii sauti inabeba hisia zangu
    Zilizomo moyoni mwangu sikia Bwana sauti yangu

    Naeleza furaha niliyo nayo
    Na hamu ya kukushukuru sikia Bwana sauti yangu.

    Nakufunulia moyo wangu uko wazi,
    Nakumiminia, sifa na tenzi Mwenyezi,
    Napiga kelele usikie Bwana sauti yangu

    Sikia aa sikia Bwana ( Mungu we)
    Sikia aa sikia Bwana sauti ya moyo,
    Moyo,moyo, wangu moyo, moyo, moyo ha ha-

    // k i i t i k i o //

    Nimejua ya kwamba - wewe ni Mungu kila wakati
    Naona wazi kwamba - wewe ni Mungu kila wakati
    Kwenye furaha - wewe ni Mungu kila wakati
    Na kwenye magumu bado- wewe ni Mungu kila wakati
    Haupungui neno - wewe ni Mungu kila wakatii


    // m a s h a i r i //
  2. Hukutaka raha zinipe kiburi -
    aeee eee ukanipimia.
    Na taabu ziliponishambulia - -
    ukafungua (Bwana) mlango nikatoka salama.
  3. Na vipaji ona hukunipa vyote -
    aaee eee ukanipimia.
    Ingawaje nilipoweka juhudi -
    ukafungua( Bwana) mlango nikatoka salama.
  4. Sikuumbwa msafi kama ulivyo,
    aaee eee ukanipimia.
    Hata hivyo dhambi iliponisonga,
    ukafungua ( Bwana) mlango nikatoka salama.

    // h i t i m i s h o //

    Yeyeyeye yeyeyeyeye yeyeyeyeyeeeeee

    Nakuja nimebeba sifa kukuzungushia
    Maana utukufu ni wako milele na milele-
    Nakuja nimebeba sifa kukuzungushia
    Maana utukufu ni wako milele na milele.

    Nakuja nimebeba shangwe, na chereko
    Nakuja nimebeba kinanda watu wakuimbie-
    Nakuja nimebeba sifa kukuzungushia
    Maana utukufu ni wako milele na milele.

    Nakuja nimebeba sifa kukupamba
    nakuja nimebeba maua jama watu wakutukuze-
    Nakuja nimebeba sifa kukuzungushia
    Maana utukufu ni wako milele na milele.

    Milele na milele, milele na milele,
    milele na milele,milele ni Mungu wa pekee...*5

    * (Bass) Wewe ni Mungu, wewe ni Bwana,
    we ni mwema, utabaki Mungu X2
    * ( Tenor) wewe ni wa kwanza ni Mungu weee, wewe ni wa mwisho eee
    Unaitwa Alfa ni Mungu wee, wewe ni Omega eee

MILELE NI MUNGU WA PEKEEEEEEE