Ni Neema

Ni Neema
Alt TitleNeema za Mungu
Performed byMoyo Mtakatifu wa Yesu UDSM
AlbumNeema za Mungu
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerZacharia Gerald
Views20,235

Ni Neema Lyrics

  1. Tunafanya kazi kwa juhudi na nguvu nyingi tena tunajituma
    Mafanikio yake tunayaona wazi kwa macho yetu
    Tunaridhika na kujiona tunafanya sisi
    Kwa nguvu na akili zetu tunasahau ya kwamba hizi ni neema

    { Ni neema (neema) mi neema (ni neema)
    Ni neema (neema) zake mwenyezi } *2 Mungu

  2. Na elimu tunapata kwa gharama kubwa tena elimu ya juu
    Na tunadhani kwamba ni akili zetu za kibinadamu
    Tunagundua vitu vipya bora na vya kisasa
    Vya kuvutia eti tekinolojia yetu imekua wapendwa
  3. Turudishe sifa utukufu na enzi kwa Mungu aliyetuumba
    Na tuwe na hofu kwake kwani yeye anatupa yote
    Tunayaweza yote katika yeye peke yake,
    Tunayaweza haya yote ni kwa yeye atutiaye nguvu kweli

    ~ ~ ~
    { Piga vigelegele*3
    Piga makofi piga vigelegele piga makofi }
    Yeye ndiye nguvu yetu, Yeye ndiye ngao yetu
    Yeye ndiye shibe yetu yeye ndiye Mungu wetu milele
    {Piga makofi} *6
    Piga vigelegele *3
    Piga makofi *3