Acheni Kukata Tamaa

Acheni Kukata Tamaa
Performed bySt. Cecilia Mirerani
AlbumMaajabu ya Mungu
CategoryKwaresma na Toba (Lent & Repentance)
ComposerBernard Mukasa
Views19,879

Acheni Kukata Tamaa Lyrics

  1. {Mwenyezi ameniumba, akanileta kati yenu,
    Niwakumbushe watu wake thamani yenu duniani} *2
    {Acheni acheni kufa moyo,
    Acheni acheni kukata tama
    Yeye aliyewaumba anaijua kazi yake } *2

  2. Aliijua siri yenu hata kabla hamjaumbwa,
    Ramani ya maisha yenu, yote imo mikononi mwake
    Magonjwa yanayowatesa na maumivu yasiyokoma,
    Ni madogo kuliko yale aliyoyaponya kwa sekunde
  3. Hali mbaya ya kiuchumi, mlo mmoja madeni mengi
    Ni njia ya kunyenyekea na kumpa Mungu ukuu
    Misiba inayowaliza mnapofiwa na ndugu zenu,
    Ni njia ya wapendwa wenu kwenda mbinguni wakafurahi
  4. Maumivu ya kuonewa kudhulumiwa kusingiziwa
    Ni nafasi ya kusamehe na kujivika utakatifu
    Matatizo ya ndoa zenu na migogoro ya familia,
    Ni bahati mmejaliwa ya kujifunza uvumilivu
  5. Bebeni misalaba yenu, nyamazeni msinung'unike
    Huo ndio wokovu wenu shikilieni msiachie