Asilegee Moyowe

Asilegee Moyowe
Alt TitleAsiregee Moyowe
Performed bySt. Joseph Cathedral Dar-es-Salaam
CategoryKwaresma na Toba (Lent & Repentance)
Composer(traditional)
VideoWatch on YouTube
Views26,759

Asilegee Moyowe Lyrics

  1. Asilegee moyowe, asitokwe machozi,
    Akimkumbuka Munguwe, kwa yake makombozi,
    Mtoa roho msalabani, mtaka kufa mwenyewe,
    Kwa sababu kumpenda ni, nani mfunga moyowe?
  2. Bustani mle Getsemani, amwomba Mungu Baba,
    Je mtu Mungu ana nini?, nguvu zake ni haba,
    Rabbi wangu waziona, dhambi za binadamu,
    Mwili wako umetona, kama jasho la damu.
  3. "Salamu Rabi salamu", anena Yuda mbaya,
    Mwenye moyo wake mgumu, ambusu pasi haya,
    Aliwaambia “basi, ntakayembusu ndiye,
    Mtwaeni na kwa upesi”, Yuda nani nisiye.
  4. Yuda nani ila yeye, aliyetenda dhambi?
    Akikosa kwa Munguwe, mtenda kwa hia na mbi,
    Mwenye kumtendea mema, mtaka dhambi haoni,
    Kwamba ni kutupa neema, kumwendea shetani.
  5. Wote ni kupiga mbio, mitumewe pamoja,
    Wamtia mikono yao, askari walokuja,
    Wampeleka hukumuni, aamuliwe na mtu,
    Ye kutoka uwinguni, Mwanzi mkuu wa watu.
  6. Mtume Petri amkanusha, amenena “simjui”,
    Uhodari umekwisha, machoye hainui,
    Pilato amwona Rabbi, hakukosa 'ta neno,
    Asema “sioni dhambi”, lakini ni mwoga mno.
  7. Athubutu kumwachia, “si hukumu” aomba,
    “Mmoja nitamfungulia, Yesu au Baraba,
    Wayahudi mwamtakani?", “Baraba aachwe tu,
    Yesu afe msalabani, damuye juu yetu”
  8. Pilato “hukumu gani? simo nanawa mkono,
    Mkimtaka Yesu mwueni”, la mwamzi hilo neno,
    Mara askari wamwanza, ni kupiga kelele,
    Kumcheka na kumchokoza, mwenye mema milele.
Asiregee Moyowe is a traditional piece. The piece has been harmonized and arranged by various composers, the most common piece being John Mgandu's harmony (1986) based on a French traditional melody, “Jésus-Christ monte qu Calvaire”. The song has been recorded by several choirs among them St. Patrick Morogoro, St. Augustine Mavurunza Dsm