Enendeni Msiogope

Enendeni Msiogope
Performed byKwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha
AlbumNakaza Mwendo (Vol 19-20)
CategoryInjili na Miito (Gospel)
ComposerFr. Mutajwaha
Views4,993

Enendeni Msiogope Lyrics

  1. { Enendeni, nendeni msiogope
    Lihubiri neno duniani pote, nendeni }*2

  2. Enyi wanafunzi wangu mimi nawatuma
    Mataifa yote nendeni mkahubiri
    Nendeni kwa moyo wote wala msiogope
    Shikeni vyema shauri ninalowapa ee!
  3. Enjili hii viumbe vyote visikie
    Ili mapenzi ya Baba yatimilike
    Nyumba, anasa na mali havina nafasi
    Ondokaneni na hivyo nimewatuma ee!
  4. Dhiki hatari na shida havitawaweza
    Giza na hila za mwovu vitayeyuka
    Elewa kwamba mimi nipo nanyi daima
    Ondoeni shaka kwani sitawaacha ee!
  5. Nanyi mkishatimiza niliyowamuru
    Posho kupata na taji mtavalishwa
    Itakuwa heri gani Mbinguni kufika
    Enzi nitakayopewa kuwarithisha ee!