Haya Karibuni

Haya Karibuni
Performed by-
CategoryEkaristia (Eucharist)
Views3,558

Haya Karibuni Lyrics

  1. Haya wapendwa wote mwaalika kwa karamu
    Kushiriki utamu, utamu wa karamu
    karamu ya Bwana *2
    Amka ndugu yangu Bwana Yesu ametuita
    Tukale mwili wake pia tukanywe damu yake
    (twende) simama simama simama
    Simama umpokee ee changamka changamka
    Changamka changamka akujaze neema zake

  2. Karamu ya mapendo karamu safi na takatifu,
    Mwaalikwa wapendwa ili mpokee
  3. Wenye mioyo safi Mwokozi sasa ametuita,
    Kwa moyo safi twende wote tupokee
  4. Tutubu dhambi zetu tushiriki karamu ya Bwana
    Kwa moyo safi twende wote tupokee
  5. Ni mapendo makubwa Mwokozi yeye katulinda
    Tuleni siku zote tufike kwake