Kazi ya Vidole

Kazi ya Vidole
Alt TitleNikiziangalia Mbingu
Performed bySt. Charles Lwanga Kisii
AlbumAsubuhi Mchana Usiku
CategoryZaburi
Views5,871

Kazi ya Vidole Lyrics

NIKIZIANGALIA MBINGU

  1. Nikiziangalia Mbingu, kazi ya vidole vyako
    Mwezi nyota ulizoziratibisha,
    (Mtu ni kitu gani (mtu ni) hata umkumbuke
    Na binadamu hata umwangalie *2)

  2. Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu
    Umemfika taji ya utukufu na heshima
    Umemtawaza juu ya kazi ya mikono yako
    Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake.
  3. Kondoo na ng'ombe wote, na ng'ombe wote pia
    Naam na wanyama wa kondeni, wa kondeni
    Ndege wa angani na samaki wa baharini,
    Na kila kipitacho njia za baharini.
  4. Wewe Mungu Bwana wetu Mungu Bwana wetu
    Jinsi lilivyotukufu jina lako duniani
    Wewe umeweka utukufu wako Mbinguni
    Vinywani mwa watoto umeweka misingi
  5. Kwa sababu yao wanaoshindana na wewe,
    Uwakomeshe adui na kulipa kisasi
    Mtu kitu gani hata wewe umkumbuke
    Na binadamu hata umwangalie