Kila Penye Ngoma

Kila Penye Ngoma
Performed byKwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha
AlbumBwana Kafufuka
CategoryHarusi
ComposerA. S. Haule
Views6,978

Kila Penye Ngoma Lyrics

  1. { Kila penye ngoma, hapakosi chereko (chereko)
    Na kila penye chereko chereko
    Zawadi zawadi hazikosi } *2

    { Twendeni sasa kwa Bwana mfufuka
    Aliyeyashinda mauti mzima kweli
    Zawadi zawadi tukatoe } *2
    { Haya twende twende twende
    Zawadi tumwage tumwage
    Kwa Bwana aliyefufuka, fufu-ka } *2

  2. Watu hutoa zawadi nzuri tena za kutamanisha
    Siku siku ya harusi, siku ya ngoma
    Je mimi nitatoa nini hata kikupendeze
    Siku siku ya kufuka, siku ya leo
  3. Bwana simama kwa chereko, nyimbo ngoma na vigelegele
    Siku siku ya kufuka, siku ya leo
    Nawe jirani twende tukatoe hata kidogo usisite
    Siku siku ya kufuka, siku ya leo