Natamani Kwenda Mbinguni

Natamani Kwenda Mbinguni
Alt TitleWatakatifu wa Mbinguni
Performed bySt. Joseph Migori
AlbumNitachezacheza
CategoryTafakari
ComposerAlfred Ossonga
Views16,403

Natamani Kwenda Mbinguni Lyrics

  1. Watakatifu wa Mbinguni
    waimba nyimbo za shangwe
    Na malaika wake Mungu
    wanarukaruka kwa shangwe
    Natamani kwenda mbinguni,
    nikaimbe nyimbo za shangwe
    Nijiunge na malaika,
    nikaruke mbele za Mungu

  2. Ewe mpenzi wa moyo, ewe mlinzi wa roho,
    Roho yangu mimi,
    Nakusihi sana ewe somo wangu, nishike mkono
    Niongoze vyema nikajiunge nawe
  3. Ee malaika wa Mungu, shuka kutoka Mbinguni,
    Njoo kwangu mimi
    Nakusihi sana nipe mbawa zako, na mimi niruke
    Nifike mbinguni nikajiunge nanyi
  4. Nyinyi mlioyashinda majaribu yake Mungu,
    Hapa duniani
    Twawasihi sana mkatuombee, na sisi tushinde
    Majaribu haya tukajiunge nanyi
  5. Matendo yaliyo mema, maneno yale mazuri,
    Moyo wa mapendo
    Zitaniongoza siku zangu zote, za maisha yangu
    Hadi nije huko nikajiunge nanyi