Nitamhimidi Bwana

Nitamhimidi Bwana
Performed bySt. Charles Lwanga Kisii
CategoryEkaristia (Eucharist)
Views5,572

Nitamhimidi Bwana Lyrics

  1. Nitamhimidi Bwana kila wakati
    Sifa zake zi kinywani mwangu daima
    Nafsi yangu itajisifu kwake Bwana
    Wanyenyekevu wasikie wafurahi

  2. Macho ya Bwana hutazama wenye haki
    Masikio yake husikia kilio
    Uso wake ni juu ya watenda mabaya
    Onjeni muone kuwa Bwana yu mwema
  3. Walilia naye Bwana akasikia
    Akawaponya na akawafuta machozi
    Yu karibu kwa waliovunjika moyo
    Onjeni muone kuwa Bwana yu mwema
  4. Mateso ya mwenye haki kweli ni mengi
    Lakini Bwana humponya nayo yote
    Huhifadhi mifupa yao yote
    Onjeni muone kuwa Bwana yu mwema