Tutalihubirije Neno

Tutalihubirije Neno
Performed bySt. Don Bosco Mirerani
AlbumRamani ya Mbinguni
CategoryInjili na Miito (Gospel)
ComposerD. P. Kweka
Views3,111

Tutalihubirije Neno Lyrics

  1. Tutalihubirije neno lake Mungu
    Huku viunoni mwetu ni mahirizi
    Neno la Mungu halifanyiwi dhihaka
    Tukaeni tukilijua jambo hili
    Tuzitoe hirizi viunoni mwetu
    Na vibuyu vilivyomo ndani ya nyumba
    Tuuteketezeni ufalme wa giza
    Tuukaribishe ufalme wa Mbinguni
    Sikieni niwaambie siri moja
    Ushirikina mwisho wake jehanamu
    Tukikabidhi maisha yetu kwa Mungu
    Tutapata mema na raha ya mbinguni

  2. Ukitazama baadhi ya familia
    Waziamini tunguri kuliko Mungu
    Ukitazama baadhi ya familia
    Wanaendesha kazi zao kwa tunguri
  3. Wakati wengine wanapoenda ibada
    Sisi wengine tunakwenda kunywa pombe
    Kutokana na malezi yao nyumbani
    Na watoto disko kulisakata rumba
  4. Ndugu zangu sasa ninawakaribisha
    Tuingie ndani ya hekalu ya Mungu
    Kabidhi kila kitu kwake Mungu Baba
    Mungu Baba ndiye mwisho wa mambo yote