Hawa Ndio Wanaotapatapa

Hawa Ndio Wanaotapatapa
Performed bySt. Don Bosco Mirerani
AlbumIkulu ya Mbinguni
CategoryTafakari
ComposerM. Z. Yohana
Views3,524

Hawa Ndio Wanaotapatapa Lyrics

  1. Hawa ndio wale wasiomkumbuka Mungu
    Ndio wale wasiomtumaini Mungu
    Wanataka maisha ya mkato pasipo kutoka jasho
    Hutamani visivyo vyao viwe vyao
    Tegemeo lao ni kwa waganga ambapo hupewa dumba
    Ili wapate kudhulumu vya wenzao
  2. Hawa ndio wale wanaotapatapa ovyo
    Ndio wale wasiomtumaini Mungu
    Kila siku ni kiguu na njia eti wasaka pesa
    Hata kukumbuka kusali hawataki
    Wamesahau ya kwamba Mwenyezi ndiye mgawa vyote
    Na ndiye mpaji wa vyote kwa wanawe
  3. Hawa ndio wale wanaomkufuru Mungu
    Ndio wanaochezea Jina lake Mungu
    Wanaishi maisha ya uzinzi pasipo kufunga ndoa
    Na maisha yao hujaa machungu mengi
    Wengine wanaharibu miili eti wawe warembo
    Kana kwamba Mungu hakuwaumba vizuri
  4. Hawa ndio wale wanaomdhihaki Mungu
    Ndio wale wasioheshimu uhai wao
    Wanatumia vibaya miili yao kwa ukahaba
    Eti ili wajipatie kitu kidogo
    Wengine wanavyolegeza ndoa sababu ya nyumba ndogo
    Na kuziacha familia zikiteseka
  5. Hawa ndio wale wanaompendeza Mungu
    Ndio wale wanaoshika njia zake Mungu
    Wale walioyatoa maisha yao kuwa sadaka
    Kwa kumtumikia Mungu kwa undani
    Wanaouthamini uhai wao pia na majirani zao
    Wakisaidiana vyema na kupendana