Hubirini Kwa Sauti

Hubirini Kwa Sauti
Performed bySt. Monica Moi Barracks
CategoryInjili na Miito (Gospel)
ComposerAlfred Ossonga
Views4,952

Hubirini Kwa Sauti Lyrics

  1. Hubirini kwa sauti ya kuimba, tangazeni haya
    Hubirini kwa sauti ya kinanda, tangazeni haya
    Yatamkeni, tamkeni hadi mwisho wa dunia
    Semeni Bwana amelikomboa taifa lake

  2. Mwimbieni Bwana wimbo ule mpya,
    Mwimbieni Bwana enyi mataifa
    Mwimbieni Bwana kwa sauti ya shangwe,
    Mwimbieni Bwana libarikini jina lake
  3. Tangazeni wokovu siku kwa siku,
    Hubirini habari za utukufu
    Yahubirini mataifa sifa zake,
    Na watu wote habari za ukuu wake
  4. Mpeni Bwana utukufu na nguvu,
    Mpeni Bwana enyi wana wa Mungu
    Pelekeni habari zake pande zote,
    Mpeni Bwana utukufu wa jina lake
  5. Mwabuduni Bwana kwa utakatifu,
    tetemekeni mbeleze nchi yote
    Semeni kwamba Bwana ametamalaki,
    Atawahukumu watu wake kwa adili