Pilka Pilka

Pilka Pilka
Performed byChrist The King Bungoma
AlbumPilka Pilka
CategoryTafakari
ComposerOchieng Odongo
Views10,974

Pilka Pilka Lyrics

  1. Pilka pilka kila siku watu wa dunia
    Wanahangaika kutafuta mali za dunia
    Asubuhi ni msongamano, mchana vilevile
    Usiku shughuli zafanyika kama kawaida

    Tafuteni kwanza ufalme ule wa mbinguni
    Na hayo mengine (hakika) mtazidishiwa
    {Yeye Mungu (Mwenyezi) mtetezi (ajabu)
    Mkiamini atawashughilikia } * 2
  2. Pilika pilika watu wengi kutafuta elimu
    Hawakumbuki kwamba Yesu ni mwalimu tosha
    Ajali nyingi barabarani zinafanyika kwetu
    Tumesahau kwamba Yesu ni dereva tosha
  3. Pilika pilika twatafuta hospitali kubwa
    Huku daktari mkuu ni Mungu wa majeshi
    Watu watafuta waganga ili wapate mali
    Bali Mungu wa mbinguni ndiye mmliki wa vyote
  4. Pilika pilika tunawaza usiku na mchana
    Vile tutakula vizuri na kuvaa vizuri
    Kwani ndege wale wa angani wanalishwa na nani
    Kama siyo Mungu wa mbinguni basi huyo nani
  5. Pilika pilika wenzangu tumuelekee Mungu
    Tusifadhaike bali tuwe na matumaini
    Atatujalia mema mengi tukiwa duniani
    Mwisho tutafurahi na Yesu kule juu mbinguni