Hiki ni Chakula kwa Wote

Hiki ni Chakula kwa Wote
Performed by-
CategoryEkaristia (Eucharist)
Views3,442

Hiki ni Chakula kwa Wote Lyrics

  1. Hiki ni chakula kwa wote wampendao
    Mkate na divai ni chakula cha Roho
    Wanyofu wa moyo twendeni tukampokee
    Tupate uzima wa milele na milele

  2. Bwana Yesu alhamisi kuu kajitolea,
    Mwili na damu yake ziwe kiburudisho
    Akatuamuru tukipenda kumkumbuka,
    Mwili na damu ni ishara ya penzi lake
  3. Alaye mwili na kunywa damu asema Bwana
    Aishi ndani yangu na mimi ndani yake
    Yeye ni rafiki yangu na nitamfufua,
    Nitaandamana naye safarini mwake
  4. Alaye mwili wa Yesu na kuinywa damu,
    Bila stahili ana hukumu ya milele
    Tujitakase kabla ya kula karamuyo,
    Kitubio ni sakramenti ya mapatano
  5. Ee Yesu nipe neema ya kukupokea,
    Unipe nguvu ya kuweza kujitakasa
    Unijalie kukupenda na moyo wote,
    Mwishowe nishiriki karamu ya Mbinguni